Warts inaweza kutokea kwenye mikono. Sehemu zilizoota vinundu ni vinyama
vilivyoota na ukiviangalia kwa makini vinamwonekano kama taulo.
Vinyama hivyo pia vinaweza kutokea usoni, hasa sehemu karibu na kope ama maeneo mengine kama vile vidole vya miguu na mikono.
Madhara
Warts inaweza kubainika kwa vipimo vya maabara.
Warts zikitokea katika shingo ya kizazi, inaelezwa kuwa inasababisha
saratani ya kizazi kwa wanawake na kwa upande wa wanaume inasababisha
kansa kwenye sehemu ya njia ya mkojo.
Anasema mtu wenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi
yupo katika hatari ya kupata ugonjwa huo kwa sababu nyama hizo huota na
kukua kwa haraka kutokana na upungufu wa kinga iliyoshuka.
Matibabu
Dk Mushi anasema licha ya ugonjwa huo kusababisha
madhara kwa binadamu, ikiwamo saratani na kukosa mtoto, lakini unatibika
ikiwa mgonjwa atawahi matibabu.
Dk Mbasa ambaye pia ni specialist wa Magonjwa ya kifua kikuu na
ukoma anasema tatizo la ugonjwa huo linaongezeka kila siku kutokana na
uelewa mdogo kwa baadhi ya jamii.
Anasema baadhi ya wanaume walio katika ndoa ambao
huomba kufanyiwa tohara katika hospitali hiyo, wengi wao wanakutwa na
ugonjwa huo na kuanzishiwa matibabu.
Mikakati kuukabili
Dk Mbasa anasema moja kati ya mikakati
inayoendelea kwa nchi nzima ni katika kupambana na ugonjwa huo ni kutoa
elimu na kuhamasisha jamii kwenda katika vituo vya kutolea tiba kwa
ajili ya uchunguzi na tiba sahihi.
“Vilevile tunaendesha kampeni za tohara kwa
wanaume kwani wanaume wanaotahiriwa hupunguza uwezekano wakupata warts
kwa asilimia 77 hadi 95, huku upande wa maambukizi ya VVU, mwanamume
ambaye amefanyiwa tohara hupunguza uwezekano wa kupata VVU kwa asilimia
60,” anasema.
Kundi hatarini
Daktari bingwa wa magonjwa ya kuambukiza na
yasiyoambukiza kutoka Kliniki ya MediCorps, Francis Makwabe anasema watu
walio na umri kuanzia miaka 14 hadi 35 wapo katika hatari ya kupata
ungojwa huo hususan wanawake waliovunja ungo na wale walikatika umri wa
kuzaa.
Dk Makwabe anasema wenye mimba wapo katika hatari
ya kupata sunzua kwa sababu mama mjamzito anakuwa na upungufu wa kinga
ya mwili.
Vilevile, anasema wagonjwa wa kisukari wapo katika
hatari ya kupata ugonjwa huo kutokana na kupungua kwa kinga ya mwili
pamoja watu wanaotumia dawa kali. Kundi jingine lililopo katika hatari
ya kupata warts, analitaja ni la wale wanaofanya mapenzi kwa njia ya
mdomo, kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja na kufanya ngono kinyume cha
maumbile.
Mbali na kundi hilo vilevile watoto wadogo wanaweza kuambukizwa ugonjwa huo kwa kufanyiwa vitendo vya ubakaji.
Dalili zake:
Moja kati ya dalili za ugonjwa huo ni kuwa na
vinyama au vinyuzi nyuzi mithili ya taulo laini katika sehemu za siri
ambapo mara nyingi huwasha wakati wa joto au unaponyoa nywele sehemu za
siri.
0 comments:
Post a Comment