Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) iliundwa kwa
tamko la Serikali la mwaka 1973, lengo kubwa likiwa kupanga mji,
kuishauri na kuisaidia Serikali kuhamia Dodoma.
Wazo la kuhamia Dodoma lililotamkwa miaka 42
iliyopita, enzi za utawala wa Rais wa Kwanza wa Tanzania, Hayati Mwalimu
Julius Nyerere, limegeuka kama wimbo machoni pa watu na linatekelezwa
kwa kusuasua. Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera,
Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama anasema azma ya Serikali kuhamia
Dodoma bado iko palepale na mchakato unaendelea.
“Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa sheria ya kuhamia Dodoma,” anasema Mhagama.
Lakini CDA iliyopewa majukumu ya kushauri katika
mradi huo inaeleza kuwa kasi ndogo ya uhamiaji wa Dodoma inasababishwa
na mtazamo wa wahusika.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CDA, Paskasi Muragili
anasema awali jukumu la kuendeleza mji wa Dodoma liliachwa kwa Serikali
Kuu pekee, huku sekta binafsi na taasisi nyingine zikiwa kando.
“Serikali imebadilisha mtazamo wake, sasa mji wa
Dodoma utajengwa na Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi,” anasema
Muragili.
“Sekta binafsi inaweza kujenga sehemu ya huduma
muhimu. Kwa hiyo Serikali haijahamia kwa sababu hakuna mazingira
yanayoiwezesha kuwa hapa Dodoma,” anasema Muragili.
Viongozi kuchochea migogoro
Akizungumzia suala la baadhi ya viongozi kuchochea
migogoro akiwamo yeye, Muragili anasema miradi mingi ya CDA imekuwa
ikikwama kutekelezwa kwa sababu ya matakwa ya kisiasa.
“Nimekuwa nikisikia kuwa nina mgogoro na CDA, lakini binafsi nikiwa nao, sioni mgogoro huo,” anasema.
Anasema tangu aliposhika nafasi hiyo, amehudhuria
vikao vya madiwani mara mbili kwa ajili ya utendaji wa mji na walifikia
makubaliano.
“Pia tumekuwa na semina ileyolenga kuzungumzia
namna tutakavyokwenda katika utendaji wa pamoja, ambapo tulifikia
maazimio fulani,” anasema Muragili na kuongeza:
Lakini zipo kauli za wanasiasa zinazokwenda tofauti na tunayotenda. Hili ndilo linanifanya nishindwe kukiri kuwa kuna mgogoro kati yetu na madiwani,” anasema.
Lakini zipo kauli za wanasiasa zinazokwenda tofauti na tunayotenda. Hili ndilo linanifanya nishindwe kukiri kuwa kuna mgogoro kati yetu na madiwani,” anasema.
Anasisitiza kuwa suala hilo ni la kisiasa na kwamba utendaji wao wa kazi umekuwa ukiungwa mkono na manispaa.
Hata hivyo, anasema changamoto kubwa nyingine ni wananchi kutofuata taratibu za uendelezaji wa Mji wa Dodoma.
Anasema kwa sasa CDA haitabomoa nyumba
zilizojengwa kinyume cha taratibu, bali cha muhimu ramani ya Mipango
Miji (Master Plan) ionyeshe kuwa eneo husika limetengwa kwa makazi.
Anasema kitakachofanyika katika maeneo hayo ni kuboresha tu na wala siyo kubomoa.
“Kama ni eneo kwa ajili ya shule, barabara au miundombinu mingine tutabomoa ili kuupanga mji,” anasema.
Akizungumzia tatizo hilo, Waziri Mhagama anawataka
viongozi kutoa kauli za busara, badala ya zile zinazoweza kuibua
uchochezi kwenye jamii.
Anasema ushirikiano wa CDA na wananchi umeimarika, hivyo kuondoa vurugu zilizokuwa zikijitokeza wakati wa upimaji wa viwanja.
Udalali wa viwanja
Akizungumzia kujitokeza kwa udalali wa viwanja,
Muragili anasema: “Ni kweli kumekuwa na tatizo la udalali wa viwanja.
Nilipoingia katika nafasi hii mwaka 2012, tulifanya uchunguzi na
kugundua kuwa sababu ya kwanza ni ukosefu wa viwanja vilivyopimwa.
Hatua yetu ya kwanza ilikuwa kuhakikisha tunapima
viwanja vingi na tumeweza kupima viwanja 10,000 kati ya hivyo 5,000
vimekwenda katika mikono ya wananchi.”
Anabainisha kuwa kwa sasa mji wa Dodoma una viwanja 5,000 vinavyoweza kutolewa hivi karibuni.
0 comments:
Post a Comment